Searching...
Jumamosi, 6 Julai 2013

MPAMBE NA MWENYEKITI WA CCM MKOANI RUVUMA ASHINDWA VIBAYA UCHAGUZI

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhjq3zEhkJ6CiIEKeEsomru72EPyFrBVhUJWPWVpxYdI9i7ksV-bWW832ZVr0YM09KVViHBTO6bU4pCxRtUZvIKNyBsPZErS40LUvliH9dEfq8FYmE1uJxceXPCY-EXZ6vhc-Itw3odohC4/s1600/Picture+010.jpg

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho akiongea kwa msisitizo


Na Muhidin Amri—Mbinga

MWENYEKITI wa chama cha Mapinduzi(ccm)mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho, amepata pigo la kisiasa kufuatia mgombea aliyempandikiza katika kinyang’anyiro cha nafasi ya mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya mbinga Alan Mahai kushindwa vibaya katika nafasi hiyo kwa kuambulia kura 13 tu licha ya jitihada kubwa zilizofanywa na mwenyekiti huyo wa ccm mkoa.

Uchaguzi huo uliofanyika  hivi karibuni, katika ukumbi wa ccm wilayani hapa ulilazimika kurudiwa baada ya ule uliotakiwa kufanyika wiki iliyopita kuvunjika kufuatia baadhi ya wanachama wa chama hicho kutoridhika kwa kuenguliwa kwa jina la mmoja wa wagombea hao Allanus Ngai ambaye ameonekana kupendwa na wanachama wengi hasa madiwani na hadi  kuchoma moto ofisi ya ccm wilaya ikiwa ni  kutaka kufikisha hisia zao kwa viongozi .
Katika uchaguzi wa juzi,dalili za kushindwa kwa Mahai  zilionekana mapema asubuhi pale baadhi ya wajumbe waliposikika wakilitaja jina la Ngai  kuwa ni mtu anayefaa kuiongoza Halmashauri ya Mbinga  kwa sasa na kukosoa utaratibu uliotumika na kamati ya siasa ya mkoa wa Ruvuma  wa kulikata jina la Ngai hadi pale vyombo vya juu ndani ya chama vilipohamuru jina ilo lirudishwe na kufanyika upya uchaguzi huo ili kunusuru kutokeo kwa vurugu.

Kuanguka huko kwa Mahai ni kama pigo kwa mwenyekiti  wa Chama mkoa, kwani katika siku za hivi karibuni ameonekana kukosa tena mvuto kwa wananchama wa chama hicho na kuanza kumnyooshea kidole juu ya mienendo yake ikiwemo tabia ya maringo na dharau aliyonayo  hasa baada ya kuchaguliwa kushika nafasi ya juu katika mkoa.

Wakizungumza na gazeti ili  mjini Mbinga mara baada ya uchaguzi huo,baadhi ya madiwani na wananchi mbalimbali waliofika eneo la  uchaguzi walipongeza hatua ya kuchaguliwa Ngai kuwa mwenyekiti mpya wa Halmashauri ya wilaya hiyo na kukosoa sera za mwenyekiti wao wa Chama Oddo Mwisho kutaka kuongoza tena Halmashauri yao kwa kumpandikiza mtu, licha ya kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri mpya ya Nyasa.
Mmoja wa madiwani hao James Stuhati wa kata ya Litumbanyosi alisema madiwani wamefanya kile walichokihitaji wananchi wa Mbinga kwani walishachoshwa na uongozi wa Mwisho ambaye alikuwa kiburi na mtu mwenye majivuno na hata kwa madiwani wenzake waliomuweka madarakani.
Kwa upande mwingine baadhi ya wananchi hao walisema,kuanguka kwa Mahai ni ishara tosha kuwa Chama cha Mapinduzi kinatakiwa kujiangalia upya na kuacha tabia iliyopitwa na wakati ambapo viongozi uwachagulia wananchi mtu wa kumpigia kura hata kama hana sifa.
Georg Badomoja alisema,huu ni mwanzo mzuri sio ndani ya chama tu bali hata katika kuinusuru Halmashauri yao kwani tayari walishakosa imani na baadhi ya watumishi wake wakiwemo wakuu wa idara(mkurugenzi Shaibu Nnunduma)ambaye anatajwa  kwa matumizi mabaya ya fedha za Halmashauri hiyo ambayo inaongoza kiuchumi katika mkoa wa Ruvuma.
“kuchaguliwa kwa huyu mzee Ngai,tuna matumaini makubwa ya fedha zetu za maendeleo,sisi wana Mbinga tulishaanza kukata tama na viongozi waliokuwepo  siku za nyuma,na tunaiomba serikali ituletee mkaguzi kutoka ofisi ya CAG aje kuangalia kama mali zetu ziko salama”alisema(Kassian nyandindi) mmoja wa mwananchi ambaye hakutaka kutaja jina lake.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!