Searching...
Jumatano, 8 Mei 2013

STEVE MC CLAREN,AVB,BENITEZ WAFUNGUKA FERGUSON KUSTAAFU



 
STEVE MC CLAREN AKIWA NA FERGUSON
Aliyewahi kuwa kocha msaidizi wa Manchester united  Steve McClaren ameiambia BBC Radio5 kwamba alizungumza siku chache zilizopita mambo mbalimbali kuhusu klabu ya Manchester lakini Sir Alex hakuonyesha dalili zozote za hiki kilichotokea sahivi "niliongea naye siku chache zilizopita,na hakuonyesha dalili zozote za hiki kilichotokea leo,kwahakika sidhani kama kuna mtu yoyote anayejua sababu ya Ferguson kujiuzulu mpaka hapo atakapoamua kusema mwenyewe au mtu wa karibu sana na familia yake…hili ni jambo la kushtukiza na kuhuzunisha sana”alisema bwana Mc Claren.
AVB AKIWA NA FERGUSON.
Kocha wa Tottenham  Andre Villas-Boas ameiambia  Sky Sports kwamba "ni mshtuko mkubwa na habari za kuhuzunisha kusikia  Sir Alex anastaafu kazi,kwa hakika ligi kuu imempoteza mwalimu bora na mkongwe ambaye alikua mfano mzuri wa kuigwa na kocha vijana kutokana na mafanikio yake katika soka…mkongwe ameondoka,nitamkumbuka milele,namshukuru kwa maneno yake ambayo ameniachia,kwa hakika ni mtu ambaye ninamuheshimu sana”alisema AVB.

BENITEZ NA BABU FEGIE
Kocha wa muda wa Chelsea Rafael Benitez ameiambia Sky Sports: kwamba  "ninapenda sana kushindana na  Sir Alex Ferguson. Ninamtakia kila la kheri na nimatumaini yangu atafurahia maisha yake nje ya soka”alisema Benitez.


0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!