Searching...
Alhamisi, 15 Agosti 2013

CHADEMA WAENDELEA KUUNGURUMA...ANGALIA WALIVYOTUA SENGEREMA NA HELCOPTA A.K.A CHOPA WAKIONGOZWA NA MBOWE

IMG_2543
Helikopta maalum iliyowabeba viongozi wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Hai, Mh. Freeman Mbowe pamoja na Mbunge wa jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika walipowasili eneo la Mnada Wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza kufanya mkutano wa hadhara wilayani humo leo mchana.
IMG_2579
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Mbunge wa Jimbo la Hai, Mh. Freeman Mbowe akizungumza na wakazi wa wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza ambapo amewaasa kushiriki katika kutoa maoni ya Katiba Mpya kwa kutumia mabaraza ili kuleta mabadiliko na mapinduzi nchini.
IMG_2610
Mwananchi wa Geita ambaye jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi akitoa maoni yake ya Katiba mbele ya wakazi na wafuasi wa Chadema ambapo wengi wao wametaka Ushuru wa Masoko ufutwe pamoja na baadhi ya kinamama kulalamikia shida ya Maji kwenye Wilaya yao.
IMG_2604
Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh. John Mnyika  akiteta jambo na mmoja wa viongozi wa Chadema Hemedi Sabula wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika leo mchana wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
IMG_2547
Pichani juu na chini ni Umati wafuasi wa Chadema na wananchi wa Sengerema waliojitokeza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Mnadi wilayani Sengerema mkoa wa Mwanza.
IMG_2596
IMG_2595
Picha juu na chini watoto nao waliojitokeza kusikiliza sera za Chadema kwenye mkutano huo leo.
IMG_2589
IMG_2623
Uwanja ukiwa umefurika wakazi wa Sengerema wakati wa mkutano wa hadhara wa Chadema.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!